Friday 5 September 2014

MLIMA KILIMANJARO: FAHAMU KUHUSU MLIMA HUU WA URITHI WA DUNIA


Mlima kilimanjaro ni mlima mrefu kupita yote hapa barani AfriKa, ni mlima wa kipekee kwani sio rahisi kukuta barafu katika ukanda wa kitropiki, lakini mlima kilimanjaro una barafu iliyo tambaa kwenye kilele chake mita kadha wa kadha na kufanya kiwe kivutio kikubwa cha watalii hapa Tanzania. Ndugu msomaji wangu wa blog hii, napenda kuku habarisha kwamba upekee wake pia ni pamoja na kuwa mlima ulio simama pekee yake bila kuwa na milima saidizi.

Mlima Kilimanjaro una urefu wa mita 5895 ambao uko kwenye uwanda wa  bonde la milima ya  mashariki. 

Image result for MT. KILIMANJARO
mlima kilimanjaro

 FATILIA MFULULIZO WA MAKALA HII


Jina la Kilimanjaro halija julikana nini hasa chanzo chake, lakini kwa tafiti nilizo zifanya neno hilo inasemekena kwamba kuna mchunguzi wa bara la Ulaya alilipata neno hilo mnamo mwaka 1860 na akaliripoti kuwa ni neno la kiswahili. Lakini chanzo kingine kiliona neno Kilimanjaro ni kilima-njaro. Kuna mtafiti mwingine aliye julikana kwa jina la Johann Krapf yeye alisema kuwa ni mlima wa  wamkubwa, au mlima wa karavani, kilima maana mlima na Jaro akimaanisha karavani.

Kwa hiyo nitaweza kusema kila mtu ana sema anavyo taka hasa hawa wakuja, ila wenyeji wa mlima huu wachaga ambao wamezaliwa wakaukuta pale wanasemaje? Tunajua kuwa kuna wachaga wa lafudhi tofauti tofauti, hii pia ina sadikika ndio chanzo jina Kilimanjaro liwe na utata juu ya maana yake. Wengine wanadai kuwa ni mlima mweupe, ambapo njaro ni weupe kama ilivyo tumika hapo awali, au wengine wanasema njaro ni mmang’ao, neon hili tunalipata katika makabila tofauti tofauti kwamfano neno njaro kwa kabila la wakamba aliandika Krapf kwamba alikuwa Jagga na aliona Kima jajeu, mlima mweupe(Kiima kyeu) ambapo neno Kilimanjaro likaanza kutumika kwa watafiti wengi.
 
Lakini hatu ishii hapo tu, tukienda mbali zaidi, wengine wanadai kuwa ni neno la Kiswahili. Kilima, tatizo lina kikuja kuwa Kilima ni hill kwa kingereza. Tukumbuke kwamba wazungu walipokuja Tanzania walikuwa hawajui lugha yetu hadhimu ya Kiswahili,  wakabadilisha mlima kwenda kilima kwa msemo jina la wa wachagga, Kibo na Mawenzi.
 
Ndugu msomaji wa makala hii, tukienda mbali zaidi Kileman sehemu ya mlima Kilimanjaro limetokana na neno Kileme likimaanisha pigwa/tekwa au Kilelema imekuwa ngumu au kushindikana. Jaro sehemu ya neno limenymbuliwa kwenye  neno Njaare, ndege au chui hususani jyaro karavani

Nisikuchoshe mpenzi msomaji ilikutaka kujua hasa ukweli wa neno Kilimanjaro, sikuishihapo nlienda mpaka uchaggani na kukutana na wazee wa Kichagga wanasema nini juu ya jambo hili,
Hapo zamani wachagga waliona mkusanyiko wa barafu, na wakaona ni vema kwenda kuchunguza nini hasa, lakini hawakufanikiwa kufika, ndipo sasa wakaja na msemo Kilemanjaare au Kilemanyaro au Kilelemanjaare wakimaanisha tumeshindwa, haiwezekani, ndege, chui, au karavani. Kwahiyo imebaki dhahania tu, sasa watu wa pwani kama wabeba mizingo walivyo kuja na wazungu walisikia wachagga wakisema kilelenjaare au kilemajyaro, kwa maana rahisi haiwezekani kuupanda mlima huu, ndipo sasa watu wa pwani waka watafsiria wazungu wakilihusisha na neno lao Kilima. Kiswahili kilipo sanifishwa waliona nivema kusawazisha na kuita Kilimanjaro.
Mlima Kilimanjaro ukawa sehemu ya miliki ya Wajerumani kipindi cha ukoloni na kwa lugha yao wakita Kilima Ndscharo
Kilelekirefu ni kibo ambacho alifika mjerumani mmoja mwaka 1889, nakukiata Kaiser-Wilhelm-Spitze mlima mrefu wa ngome ya Ujerumani, tulipo pata uhuru kilele kikabadilishwa jina na kuitwa kilele cha Uhuru.

Imeandikwa na Fredy Michael
 

No comments:

Post a Comment